Tuesday 21 February 2017

FID Q HAWEZI FREESTYLE – Young Killer


YOUNG KILLER AMTOLEA POVU NGOSHA

Rapa Young Killer Msodoki amefunguka na kusema hajawahi kumkubali rapa Fareed Kubanda  Fid Q kwenye kufanya mitindo huru kwa kuwa hajawahi kumuona mkali huyo wa hip hop Bongo akifanya mitindo huru.
Young Killer alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema yeye anawakubali sana Nikki Mbishi, Godzilah pamoja na marehemu Albert Mangwea kwa kufanya ‘Free style’ sababu anatambua uwezo wao katika nyanja hiyo.
“Sijawahi kumkubali Fid Q kwa ‘free style’ sababu sijawahi kumuona akifanya hivyo ila niliowahi kuwaona wakifanya mitindo huru nampenda sana Nikki Mbishi, GodZillah pamoja marehemu Albert Magwea” alisema Young Killer
Mba na hilo Young Killer amesema baada ya kufanya kazi na Fid Q msanii mwingine wa hip hop anayetamani kufanya naye kazi kwa sasa ni Mbunge wa mikumi ‘Prof Jay’.
“Kiukweli kabisa kwa sasa hivi mimi natamani sana kufanya kazi na Prof Jay, hata hivyo tayari nipo kwenye mipango ya kufanya kazi na rapper Chemical “. Aliongeza  Young Killer.
eatv.tv

Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    4 months ago
Powered by Blogger.