Showing posts with label BURUDANI. Show all posts
Showing posts with label BURUDANI. Show all posts

Tuesday, 21 February 2017

FID Q HAWEZI FREESTYLE – Young Killer


YOUNG KILLER AMTOLEA POVU NGOSHA

Rapa Young Killer Msodoki amefunguka na kusema hajawahi kumkubali rapa Fareed Kubanda  Fid Q kwenye kufanya mitindo huru kwa kuwa hajawahi kumuona mkali huyo wa hip hop Bongo akifanya mitindo huru.
Young Killer alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kusema yeye anawakubali sana Nikki Mbishi, Godzilah pamoja na marehemu Albert Mangwea kwa kufanya ‘Free style’ sababu anatambua uwezo wao katika nyanja hiyo.
“Sijawahi kumkubali Fid Q kwa ‘free style’ sababu sijawahi kumuona akifanya hivyo ila niliowahi kuwaona wakifanya mitindo huru nampenda sana Nikki Mbishi, GodZillah pamoja marehemu Albert Magwea” alisema Young Killer
Mba na hilo Young Killer amesema baada ya kufanya kazi na Fid Q msanii mwingine wa hip hop anayetamani kufanya naye kazi kwa sasa ni Mbunge wa mikumi ‘Prof Jay’.
“Kiukweli kabisa kwa sasa hivi mimi natamani sana kufanya kazi na Prof Jay, hata hivyo tayari nipo kwenye mipango ya kufanya kazi na rapper Chemical “. Aliongeza  Young Killer.
eatv.tv

Share:

Nay wamitego atangaza nia ya kuanzisha kanisa.


Tuesday, February 21, 2017

Msani wa bongo fleva Nay wa mitego atangaza nia yake ya kuanzisha kanisa takatifu. 
 
Anadai kua kanisa lake halitakua la upigaji wa mkwanja kama makanisa feki yanavyofanya.
 
“Acha kanisa likamilike, mwenye Mungu asimamie tutajua nini kinaenda kutokea lakini sio kanisa kwaajili ya kupiga hela,” Nay aliiambia E-News.
 
Nay amedai kuwa mchungaji wa kanisa lake atakuwa tofauti na hatotegemea sadaka za waumini ili kuendesha maisha yake, bali kazi yake nyingine itakayoweza kumuingizia kipato.
Rapper huyo amejinadi kuwa anatarajia kupata waumini wengi kupitia kanisa lake na kwamba litakuwa chanzo cha mafanikio katika mambo yao.
 
Nay amedai kuwa kanisa lake litajengwa Mbezi ya Kimara jijini Dar es Salaam.

Share:

Tuesday, 27 September 2016

Familia ya Diamond Yaikacha Sherehe ya Birthday ya Zari Iliyofanyika Zanzibar...Mabifu Yaibuka Upya

Familia ya Diamond Yaikacha Sherehe ya Birthday ya Zari Iliyofanyika Zanzibar...Mabifu Yaibuka Upya

MWISHONI mwa wiki iliyopita (juzi Ijumaa usiku) ilifanyika pati ya kusherehekea kuzaliwa kwa mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari’ ambayo imeibua mabifu upya. Pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa wachache kutoka Bongo ambao ni pamoja na Moze Iyobo, Aunt Ezekiel na wengineo ilifanyika Zanzibar ambapo licha ya kufana, imeibua mtifuano upya kati ya Zari na wifi yake, Esma Abdulkadiri na Diamond na mume wa zamani wa Zari, Ivan Semwanga.
 
IVAN NA DIAMOND
Bifu la wawili hawa lilikuwa limezimika, lakini lilirudi upya baada ya juzikati Diamond kumzawadia Zari nyumba iliyopo Afrika Kusini kisha kumrushia Ivan dongo kwa kuandika mtandaoni: “Wanakazana kujisifu matajiri ilhali watoto wao wanaishi kwenye nyumba za kupanga… halafu leo yuleyule wanayemtukana kutwa kwenye mitandao kuwa maskini, kajawa na shida, kanunua nyumba kulekule kwao ili watoto wao waishi maisha bora kama wanayoyatamani… Heri ya siku ya kuzaliwa Mama tee wangu…. Nakupenda sana na unalifahamu hilo…natumai umeipenda nyumba yetu hii mpya South Africa.”

NI DONGO KWA IVAN
Ujumbe huo moja kwa moja u l i o n e k a n a kumhusu Ivan ambaye kipindi cha nyuma kwa kushirikiana na mshikaji wake aliyefahamika kwa jina la King Laurence, walikuwa wakimtusi wakimsema kuwa ni maskini ila wao wana pesa licha ya madai kuwa, nyumba wanayoishi watoto wa Zari kule Sauzi ni ya kupanga. Baada ya dongo hilo, hali ilichafuka huku Ivan akimrushia madongo Diamond sambamba kumtaka Zari amwambie bwana wake (Diamond) aondoe ujumbe huo mtandaoni kwani hata wanaye wakiuona wataumia. Inadaiwa kuwa, licha ya Ivan kuomba hivyo, Zari alimjibu kuwa Diamond amegoma kwa maelezo kwamba, wao (King Laurence na Ivan) ndiyo walioanza kumtusi.

 ESMA NA ZARI
Bifu lao lilihusishwa baada ya Esma kuulizwa sababu za kutomuwish wifi yake katika siku yake ya kuzaliwa, kuonesha ‘analo na limemfika hapa’ alifunguka: “Siwezi kumuwishi, mbona Taraj (mwanaye) hakumuwishi wakati ndiye aliyekuwa akicheza na mwanaye (Tiffah) nyumbani? Wee ukosane na mimi umkasirikie hadi mtoto, ujinga huo. Siwezi kumuwishi Mbona Bi. Snura (mama wa Diamond) alimuwishi akamfuta na mafumbo juu, akasababisha watu wakamchamba!….. (anataja jina la mwandishi) nimekaa tumboni kwa mama yangu miezi 9 ‘so’ mtu anavyomletea dharau siwezi kumpenda. Mbona wote tumekaa nao vizuri haijawahi tokea haya mambo, kwa nini yeye?” alihoji Esma.

FAMILIA YA DIAMOND YASUSA BETHIDEI
Katika kile kinachoonesha kuna kitu kizito nyuma ya pazia kati ya Zari na ndugu wa Diamond, inadaiwa hakuna hata mmoja aliyefika hali iliyoibua maswali mengi.

DIAMOND, ZARI VIPI?
Kufuatia kuibuka kwa mabifu hayo sambamba na figisu nyingine, gazeti hili lilifanya jitihada za kuwatafuta Diamond na Zari kupitia simu zao za mkononi ili waseme lolote, lakini simu zao hazikuweza kupatikana.
Share:

Saturday, 20 August 2016

Diddy na Cassie waachana rasmi baada ya ugomvi


cassie-diddy
Vyanzo vilivyo karibu na wawili hao, vimeuambia mtandao huo kuwa yalizuka mabishano makali kati yao wakiwa kwenye gari Jumatano mchana baada ya Cassie kumwambia Diddy kuwa anataka waachane. Wamesema kuwa Diddy alikasirika kiasi cha kushika simu yake na kuanza kuangalia vitu vilivyomo.
Vyanzo hivyo vimesema kuwa Diddy aliruka kutoka ndani ya gari huko Bev Hills akiwa na simu mkononi na Cassie kuondoka na dereva.
Hatimaye Diddy alirejea nyumbani na kuipeleka simu lakini baadaye akachukua magari mawili yaliyokuwa yameegeshwa nje.
Cassie alikuwa amemuambia mama yake kuhusu tukio la simu kabla Diddy hajarejea nyumbani na kuirejesha na hivyo aliwaita polisi. Polisi walifika nyumbani kwa Cassie na kuwaeleza kuwa ameipata simu yake na wakaondoka japo waliandika ripoti ya tukio hilo. Hata hivyo hakuna kosa lililofanyika.
Kuhusu kuachana, wawili hao wamewahi kuachana kabla
Share:


Share:

Tuesday, 28 June 2016

UTAJIRI WA MOND NI ZAIDI YA 8.6 TZ BILLIONS OF MONEY

Kumekuwepo na tetesi nyingi kuhusu utajiri wa Diamond umefikia kiasi gani. Hilo ni swali ambalo hajawahi kulijibu kwa uhakika zaidi ya kutoa tu hints na kuwaacha wanaouliza kubaki na majibu yao wenyewe vichwani.

Lakini kupitia kipindi maalum cha kituo cha runinga cha E!TV, E Vip kilichorushwa Jumapili ya June 26, tunaweza kusema walau kwa uhakika staa huyo ana utajiri mkubwa kiasi gani. Diamond ana utajiri wa dola milioni 4 za Kimarekani ambao kwa shilingi ya Tanzania ni zaidi ya bilioni 8.6.

Si kitu kinachoshangaza tena kwa Diamond kutokana na hatua aliyofikia akiwa msanii anayelipwa fedha nyingi zaidi Tanzania kwa sasa. Fedha zake nyingi zinatokana na show zake zisizokauka za ndani na nje ya nchi, mikataba ya ubalozi na matangazo kutoka makampuni kama Vodacom, Cocacola, DSTV na Red Gold. Hivi karibuni alipata deal jingine la kutangaza huduma ya taxi ya Uber.

Pia amekuwa akiingiza fedha nyingi kupitia biashara ya nyimbo zake hasa miito ya simu, malipo ya mirabaha kutoka nchi za jirani kama Kenya bila kusahau biashara za mtandaoni zikiwemo Youtube.

Uwekezaji wake kwenye label ya WCB ni kitu kingine kikubwa ambacho kitaanza kumuingizia fedha nyingi siku za usoni. Hadi sasa amesaini wasanii wanne wakiwemo Rich Mavoko, Raymond, Harmonize na dada yake Queen Darleen.

Lakini pia staa huyo anafahamika kwa kuwekeza zaidi fedha kwenye ardhi na nyumba huku akidaiwa kumiliki maeneo mengi jijini Dar es Salaam.
Share:

Monday, 27 June 2016

mdundo mpya wa linex ft Bellah umetoka rasmii pakuu

:)
Share:

Thursday, 23 June 2016

Nyota ya Vanessa Mdee Yazidi Kung'aa Kimataifa..Sasa kuwania Tuzo Nigeria



Msanii wa Bongofleva Vanessa Mdee jina lake limeingia kwenye headlines baada ya kutajwa katika moja kati ya tuzo kubwa Nigeria Entertainment, Vanessa ametajwa kuwania tuzo zinazoitwa Nigeria Entertainment Awards.

Jina la muimbaji Vanessa Mdee limetajwa katika kipengele cha kuwania tuzo ya muimbaji bora wa kike, katika kipengele hicho Vanessa anawania tuzo hiyo na wasanii wengine saba kutoka nchi mbalimbali, Nigeria Entertainment Awards zitafanyika New York Marekani, September 4 2016
Share:

AFANDE ADAI KUWAPIMA BADO MADEMU ZAKU


JIULIZE SASA JUPI MKE SAHIHI KWA AFANDE SELE. 
USINIULIZE KUHUSU MAMA T.
Msanii wa muziki na mwanasiasa kutoka mji kasoro bahari, Afande Sele amefunguka na kusema kuwa kwa sasa yeye hatarajii kuoa kwani bado yupo yupo sana ingawa anakiri wazi kuwa yupo na mahusiano na wanawake kama sita hivi ambao wanamsaidia kumtunzia

watoto wake huku akiangalia kati ya watu hao alionao yupi anastahili kuwa malkia.
Afande Sele alisema hayo kupitia kipindi cha Planet Bongo ya Eat Africa Radio na kusema kwa sasa yeye kusema atafunga ndoa itakuwa ni uongo mkubwa kwani watu alionao anaona bado wanapimana maana wao wanampima yeye na yeye anawapima wao na kuona yupi anastahili kuingia ndani kama mke.

"Niwe mkweli tu hilo wazo la kuvuta jiko sina, namshukuru Mungu nimepata watoto wawili naweza kwenda nao vizuri na kuwalea, kusema nifunge ndoa leo au kesho utakuwa uongo sababu ndoa si kusema mwanamke kuchukua nyanya tu gengeni,lazima nipate mwanamke amabaye atakuwa na vigezo vya kuwa na mimi atajua nini maisha ambayo mimi nayahitaji, atanielewa tabia zangu za nje na ndani hivyo sidhani kama ni rahisi kupata mke kwa kipindi hiki ila najivunia kuwa na marafiki ambao wanasaidia kulea watoto wangu, wanawapenda watoto zangu hicho nashukuru" alisema Afande Sele.

"Nipo kwenye kupima nawapima na wao wananipima mimi, mimi na marafiki wa hivyo wakati ukifika nikiona yupo anafaa kuwa na mimi nitakuwa naye lakini niwe mkweli, siko mwenyewe au kusema natumia sabuni hapana mimi na warembo kama kawaida, wananisaidia kukaa na watoto wangu, wanaheshima. Maana mimi ni kama mfalme hata mfalme Suleman alikuwa wa wake zaidi ya mia tatu kwenye nyumba yake, hata mimi wapo kadhaa ila hawazidi sita" aliongeza Afande Sele
Share:

Monday, 20 June 2016

wastara apiga chini maswala ya uigizaji

Dar es Salaam: Staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amejipanga kuachana na uigizaji na kufanya ishu nyingine ikiwa ni pamoja na biashara ambazo ameanza kuzifanya.

Akizoza na Wikienda, Wastara alisema kuwa anamalizia kazi ya uigizaji mwaka huu na mwaka unaokuja atakuwa mwingine kabisa kwani baada ya kufika nchini Msumbiji (aliko kwa sasa) amepata dili lingine zuri ambalo ataliweka wazi baada ya mipango yake  kukamilika.

“Kinacho niachisha uigizaji si biashara tu bali ni pamoja na dili nililolipata huku Msumbiji, kama litakwenda nilivyopanga, nitaliweka wazi inshallah,” alisema Wastara.

Hivi karibuni, Wastara aliripotiwa kuwa na ujauzito ambapo alikimbilia nchini Msumbiji.

Share:

Sunday, 19 June 2016

HATIMAYE MASTER J WA MJ RECORD, KURUDI KAIZNI.


Share:

Saturday, 18 June 2016

LIONE BIFU LA NAHREEL NA WEUSI WAZEE WA GEREEEE


Hivi karibuni kumeibuka taarifa kuwa ule ukaribu uliokuwepo mwanzo kati ya kundi la Navy Kenzo na Weusi umepotea tangu yalipofanyika mabadiliko ya studio ya The Industry. Nahreel amesema hilo siyo kweli bado ni washkaji kama zamani tofauti watu wanavyowachukulia.

Navy Kenzo na Weusi wamekuwa watu wa karibu sana hali iliyopelekea watu kuona wivu kwa kusema kuwa Nahreel anawapendelea wasanii hao kwa kuwatengenezea beat nzuri zaidi ya wasanii wengine.

Akiongea na Bongo5, Nahreel amesema kuwa wao na Weusi bado ni washkaji na bado wana kazi zao kwenye studio yake hazijatoka.

“Ni kweli utaratibu umebadilika na mimi kama mfanyabiashara mwingine lazima kila siku niendelee kuweka utaratibu fulani,” alisema Nahreel.

“Hapa kati nimekuwa busy na ratiba zangu na focus na Navy Kenzo tumekuwa tuna move hapa na pale kwahiyo unajua Weusi na wao wana mipango yao kama wana muziki siwezi nikawa mimi tu nawacheleweshea time zao, na hapa wana nyimbo nyingi zipo bado hazijatoka,” aliongeza.

Hata hivyo Mei 6 mwaka huu Navy Kenzo walifanya sherehe za kuzindua studio yao ‘The Industry lakini hakuna hata msanii mmoja wa kundi la Weusi aliyehudhuria sherehe hizo.
Share:

Tuesday, 14 June 2016

Daah! LIL WYNE ANAUGUA KIAFAFA, jioneee

Rapper machachari na mtalamu wa kuflow kwa makeke lil wayne amesumbuliwa tena na kaugonjwa kake ka kuanguka kifafa.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, ndege binafsi aliyokuwa amepanda rapper huyo, ililazimika kutua kwa dharura huko Omaha, Nebraska Jumatatu hii. Weezy alikuwa akisafiri kutoka Milwaukee kwenda California pindi tukio hilo lilipotokea.

Wayne alidaiwa kuzimia akiwa kwenye ndege na kupewa huduma ya kwanza. Hata hivyo ripoti zimedai kuwa alikataa kutibiwa. Taarifa zimedai kuwa alipata tena kifafa cha pili baada ya ndege yake kupaa na ililazimika arudishwe Omaha. Alipoteza kabisa fahamu na alipelekwa hospitali kwa ambulance.

Tunechi aliwahi kupata tatizo kama hilo mwaka 2012 baada ya ndege binafsi kutua kwa dharura kwa siku mbili mfululizo. Pia aliwahi kupata kifafa kikali mwaka 2013.

Share:

MH PRF JAY AIBUKA WCB KUPIGA CHABO

haya sasa kutana na Mond Bin Ladeen Bin minyota almaarufu rais wa WCB, akiwa na Mbunge wa Mikumi, Professor Jay

 Mbunge wa Mikumi ambaye ni msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop, Joseph Haule ‘Professor Jay’ Jumatatu hii alitembelea ofisi za WCB na kujionea uwekezaji uliyofanywa na rais wa label hiyo Diamond Platunmz.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Professor Jay amemsifia Diamond kwa uwekezaji aliyoufanya.

“Kikubwa kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza Diamond kwa kuwa na mawazo mapana zaidi kwa sababu kiukweli kwa wasanii wengi wa Tanzania na Waafrika wengi tunaweza tukawa na kipaji lakini mazingira yetu ya kazi yanakuwa magumu,” alisema Professor.

Aliongeza, “Kwa mfano pale kwa Daimond jana nimeenda nimekuta kuna studio hapo hapo, pamoja na kurecord lakini pia anachumba ambacho amekitengeneza cha kutengeneza photoshoot. Lakini pia ana sehemu ya kufanya editing ya kazi zake na ana watu special ambao amewaajiri kwa ajili ya kazi hizo, hii ni hatua kubwa sana kwa msanii,”

 Babu Tale akiwa na Professor Jay
 Professor Jay akiwa na Dogo Janja
Professor Jay na Raymond


Share:

Saturday, 11 June 2016

STAR WA MOVIE ZA KIBONGO SHAMSA ASEMA ANAPENDA CHUPI NA TAIT ZA MTUMBA

MWANADADA SHAMSA FORD STAR WA MOVIES ZA KISWAHILI HAPA BONGO AVUNJA UKIMYA RASMI NA KUFUNGUKA MBELE YA MEDIAS KWAMBA YENYE NI MDAU NAMBARI MOJA WA CHUPI NA SKIN TAIT ZA MTUMBA, AMESEMA HAYO BAADA YA KUONEKENA KILA STAA ANAJISIFIA KWA VIWALO VYA SPESHO TU TENA VYA BEI NDEFU SHAMSA KAFUNGUKA KIUTAMU UTAMU MBELE YA CAMERA ZETU.
 
PICHA NA MVUNGI K.A
SHAMSA12
Share:

ZIFAHAMU ADHABU ZA WASANII WA WCB


Uongozi wa label ya ‘WCB’ umesema umejipanga kikamilifu kudhibiti swala la nidhamu kwa wasanii wake
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni, mmoja kati ya viongozi wa juu wa label hiyo, Babu Tale amesema wao kama uongozi watasimama kidete kuhakikisha wasanii wa WCB wanakuwa mfano wa kuigwa kwa jamii.
“Nikijibu hapo kwenye eneo la nidhamu ni kwamba, sisi ni vijana ambao tunaishi na vinaja ambao wametoka kwenye familia zao ambazo zinamalezi tofauti tofauti, lakini wakija hapa ni lazima wafuate sheria zetu. Sitaki kumsifia Dioamond ni mtu ambaye hana nidhamu ya kuigiza, kwa hiyo hawa wengine lazima wafuate tabia za kaka yao,” alisema Babu Tale.
Aliongeza, “Kwetu msanii akitukana kwenye social network , akitukana kwenye stage huyo lazima sisi tumuadhibu. Kuna adhabu ambayo inasukumwa na social network hiyo hatuizingatii kwa sababu kila mmoja ana mapenzi yake na wengine wanachuki zao. Adhabu ambayo tatizo linaonekana wazi kwamba hili ni tatizo, tunayaita matendo kusudi, kiofisi huwenda mtu akasimamishwa bila jamii kujua, kukata pesa kwenye kazi zake bila jamii kujua, hayo mambo tunafanyia hata sisi viongozi pale tunapokosea,”
Share:

Friday, 10 June 2016

BARAka DA PRINCE AMSALITI NAJ KWA LINAH SANGA


 Barakah da Prince na mpenzi wake, Naj.

Juzikati wasanii Baraka Andrew ‘Barakah da Prince’ na Estelina Sanga ‘‘Linah’ walinaswa wakiwa kimahaba, tukio lililoibua gumzo na wengi kudhani mkali huyo wa ngoma ya Siwezi kachepukia kwa ndege mnana.

Barakah da Prince na Linah.

Baraka na Linah walinaswa katika viunga vya Escape One kulikokuwa na shoo ya Christian Bella ambapo jamaa alionekana akimshikashika mdada huyo bila aibu.

Akilifungukia tukio hilo, Baraka alisema kuwa, yalikuwa ni mapozi ya kawaida tu na wala watu wasihisi anachepuka na Linah.

“Hivi nimsaliti Naj (Najma mpenzi wake wa sasa) sijipendi? Yale ni mapozi ya kawaida tu. Narudia tena, nampenda sana Naj na hakuna mbadala wake,” alisema Baraka.
Share:

Thursday, 9 June 2016

KIM KADASHIANA AFANYA KUFURU YA KIATU CHA LAKI 7

 MWANAMITINDO na Mtangazaji wa Kipindi cha Keeping Up With The Kardashians, Kim Kardashian hivi karibuni alimfanyia sapraizi shabiki wake baada ya kumzawadia kiatu toleo la Yeezy Boost 750 chenye thamani ya shilingi laki saba za Kibongo.

Yeezy Boost 750

  Mwanadada Kim ambaye ni mama wa watoto wawili aliozaa na mumewe ambaye ni rapa, Kanye West aliandika katika ukurasa wake wa twitter.

“Vema, leo imekuwa bahati kwako… Saizi ipi inakufaa, nimekutafutia namba 10! Msaidizi wangu atawasiliana chemba na wewe kupata mawasiliano yako na Yeezy itasafirishwa kwako.”

Kiatu cha Yeezy Boost 750 bado hakijatoka, kitatoka Juni 11, mwaka huu na Kim aliweka tangazo kwenye Twitter yake kama hamasa kwa mashabiki kwa mtu atakayetoa ‘posti’ bora ya kukitangaza.
Share:

Wednesday, 8 June 2016

MALI ZA MASANJA HALI TETE, TOBA WE!

 Mwimba nyimbo za Injili na mchungaji, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji.

2016, kazi imepamba moto! Zoezi linaloendelea kufanywa na maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) la kuhakikisha kila mtu analipa kodi inavyotakiwa ili kuipa hazina mapato, sasa limetua kwa mchekeshaji, mwimba nyimbo za Injili na mchungaji, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji,’ tembea na Ijumaa Wikienda.

Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, mfanyakazi mmoja wa TRA Tawi la Kinondoni, Dar (jina lipo) alisema mamlaka hiyo imebaini kuwa, mastaa wengi Bongo na watu wa kawaida, wamekuwa wakinunua magari kimagumashi (kukwepa kodi), hivyo wameamua kuanza kuwasaka watu hao.

 Mjengo anaomiliki Masanja.

TWENDE NA CHANZO
“Mtu kama Masanja, tuna taarifa ana magari kama sita, tena mengine ya bei mbaya. Lakini ukimtafuta kwenye system (mfumo) hakuna jina lake. Sasa sijui anatumia jina gani kulipia kodi ya magari hayo.”

KUNA NINI KWANI?
Chanzo hicho kiliendelea kuweka wazi kuwa, hivi karibuni katika uchunguzi wao, TRA walibaini kuwa, msanii huyo amenunua gari la kifahari aina ya Toyota Land Cruiser Super Charger lenye thamani inayokadiriwa kufikia shilingi milioni mia mbili (200,000,000).

ANATANUA NALO MITAANI
“Masanja anatanua na gari hilo mitaani bila wasiwasi. Sisi tulimwangalia kwenye system hatumuoni.
Kuna wakati tuliamini huenda analipia kodi kwa jina la Masanja maana sisi tunajua anaitwa Emmanuel,” alisema mfanyakazi huyo.

MASANJA ANASAKWA
Mtumishi huyo akaongeza: “Tumeshaenda nyumbani kwake, Tabata Aroma karibu mara tatu lakini hatujamkuta. Tunakuta ndugu zake tu. Lengo letu ni kuona document (nyaraka) ili tujue uhalali wake katika umiliki wa magari hayo.”

 MASTAA, WATU WA KAWAIDA WAMO
“Lakini zoezi hili la kukamata magari ya wamiliki waliokwepa kodi si kwa Masanja tu, mastaa wote wamo lakini pia na watu wa kawaida.

Hapa lengo si majina bali ni serikali ya Magufuli inataka mapato. Si unajua malengo ya serikali ya awamu ya tano ni mengi, bila mapato hayatatimia na Magufuli si unajua anavyotumbua majipu, hatutaki kutumbuliwa sisi.”

MASANJA AONGEA NA WIKIENDA
Ili kuweka sawa mzani wa habari hii, Ijumaa Wikienda lilimsaka kwa njia ya simu, Mchungaji Masanja na kumuuliza kuhusu madai hayo ambapo alisema:

“Kwanza mimi sina taarifa za kutafutwa. Kama ni watu kuja kuniulizia nyumbani kwangu ni wengi sana kwa siku. Ikitokea wakaja, nitamalizana nao juu kwa juu maana sioni kama kuna sehemu nimekwenda kinyume na utaratibu wa serikali kuhusu mapato yao. Halafu mimi sina utajiri wa kiasi hicho.”

Akiwa na moja  ya mkebe anaomiliki.

WEMA ALISHAKUMBANA NAO
Mwezi mmoja uliopita, staa wa sinema za Bongo, Wema Sepetu alidaiwa kukumbana na rungu la TRA kuhusu ushuru wa gari aina ya Range Rover Evogue ambalo alilinadi kwenye sherehe yake za kuzaliwa kwamba alilinunua jipya kwa shilingi milioni mia mbili.

Wema alikiri kuzukiwa na watu hao huku akisema msaidizi wake (hakumtaja jina) ndiyo alimalizana na watu hao wa TRA.

WOLPER ALISIKIA
Mbali na Wema, mcheza filamu mwingine wa Bongo, Jacqueline Wolper naye aliwahi kuzungumza na gazeti hili na kusema amesikia watu wa TRA wameanza kuwasaka mastaa wa Bongo kuhusu ushuru wa magari wanayomiliki.

Alhamisi iliyopita, gazeti hili lilitinga kwenye ofisi za TRA Tawi la Kinondoni maeneo ya Mwenge, Dar ili kupata mzani wa habari hiyo lakini hakufanikiwa kumpata msemaji kufuatia kila ofisa aliyefikiwa kudai siyo msemaji wa mamlaka hiyo.
Share:

Tuesday, 7 June 2016

BOOOM!!!!!! UDOM AGAIN

Wapendwa watu wetu tunapenda kutangazia kuwa zoezi la kusain Fedha za kujikimu litaendelea kesho siku ya jumatano fikeni bila kukosa.
Share:

MWONE WOLPER NA HII TENA

Share:

Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

Powered by Blogger.