Thursday 9 June 2016

KODI ZA KUSAJILI GARI KWA JINA ZA ZIDI KUPANDA ZAIDI YA 5 MILLION



Bajeti ya Serikali iliyotangazwa huenda ikapunguza idadi ya watu wanaopenda kuonekana tofauti, kwenye usajili wa magari kwa kuandika majina yao badala ya namba.

Wamiliki wa magari wanaotaka kusajili namba binafsi kama kuweka majina yao, sasa watalipa Sh10 milioni badala Sh5 milioni za awali, kwa kipindi cha miaka mitatu.

Akitoa mapendekezo ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka 2016/17 jana, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango aliomba Bunge liridhie kufanya marekebisho ya Sheria ya Magari (Kodi na uhamisho wa umiliki) ili kupandisha usajili wa namba hizo.

Namba hizo binafsi zilizoanzishwa miaka minne iliyopita, zinaruhusu mtumiaji kuandika jina au neno lolote kwenye gari lake tofauti na namba za kawaida zinazotumika nchini.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.