Saturday 18 June 2016

LIONE BIFU LA NAHREEL NA WEUSI WAZEE WA GEREEEE


Hivi karibuni kumeibuka taarifa kuwa ule ukaribu uliokuwepo mwanzo kati ya kundi la Navy Kenzo na Weusi umepotea tangu yalipofanyika mabadiliko ya studio ya The Industry. Nahreel amesema hilo siyo kweli bado ni washkaji kama zamani tofauti watu wanavyowachukulia.

Navy Kenzo na Weusi wamekuwa watu wa karibu sana hali iliyopelekea watu kuona wivu kwa kusema kuwa Nahreel anawapendelea wasanii hao kwa kuwatengenezea beat nzuri zaidi ya wasanii wengine.

Akiongea na Bongo5, Nahreel amesema kuwa wao na Weusi bado ni washkaji na bado wana kazi zao kwenye studio yake hazijatoka.

“Ni kweli utaratibu umebadilika na mimi kama mfanyabiashara mwingine lazima kila siku niendelee kuweka utaratibu fulani,” alisema Nahreel.

“Hapa kati nimekuwa busy na ratiba zangu na focus na Navy Kenzo tumekuwa tuna move hapa na pale kwahiyo unajua Weusi na wao wana mipango yao kama wana muziki siwezi nikawa mimi tu nawacheleweshea time zao, na hapa wana nyimbo nyingi zipo bado hazijatoka,” aliongeza.

Hata hivyo Mei 6 mwaka huu Navy Kenzo walifanya sherehe za kuzindua studio yao ‘The Industry lakini hakuna hata msanii mmoja wa kundi la Weusi aliyehudhuria sherehe hizo.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.