Uongozi wa label ya ‘WCB’ umesema umejipanga kikamilifu kudhibiti swala la nidhamu kwa wasanii wake
Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni, mmoja kati ya viongozi
wa juu wa label hiyo, Babu Tale amesema wao kama uongozi watasimama
kidete kuhakikisha wasanii wa WCB wanakuwa mfano wa kuigwa kwa jamii.
“Nikijibu hapo kwenye eneo la nidhamu ni kwamba, sisi ni vijana ambao
tunaishi na vinaja ambao wametoka kwenye familia zao ambazo zinamalezi
tofauti tofauti, lakini wakija hapa ni lazima wafuate sheria zetu.
Sitaki kumsifia Dioamond ni mtu ambaye hana nidhamu ya kuigiza, kwa hiyo
hawa wengine lazima wafuate tabia za kaka yao,” alisema Babu Tale.
Aliongeza, “Kwetu msanii akitukana kwenye social network , akitukana
kwenye stage huyo lazima sisi tumuadhibu. Kuna adhabu ambayo inasukumwa
na social network hiyo hatuizingatii kwa sababu kila mmoja ana mapenzi
yake na wengine wanachuki zao. Adhabu ambayo tatizo linaonekana wazi
kwamba hili ni tatizo, tunayaita matendo kusudi, kiofisi huwenda mtu
akasimamishwa bila jamii kujua, kukata pesa kwenye kazi zake bila jamii
kujua, hayo mambo tunafanyia hata sisi viongozi pale tunapokosea,”
0 comments:
Post a Comment