Tuesday 7 June 2016

ARGENTINA YA MCHAPA CHILE GOLI 2-1 COPA AMERICA

leo Alfajiri katia mechi ya kukata nashoka baina ya Argentina na Chile kwenye michuano ya COPA AMERICA inayorindima kunako bara la Marekani.
 
Argentina walijipatia bao la kwanza dakika ya 50 kupitia kwa mshambuliaji wa pembeni anayekipiga kunako klabu ya PSG, Angel Di Maria, dakika 9 baadaye Chile walifanya chambulio la nguvu langoni mwa Argentina lakini halikuzaa goli na papo hapo Argentina wakatumia mwanya huo kufanya 'Counter Attack' langoni mwa Chile na bila ajizi Ever Banega akatumbukiza bao la pili, na kufanya ubao wa matokeo kusomeka 2-0. Katika dakika za majeruhi Jose Fuenzalida akaipatia Chile bao la kufutia machozi. Mwisho wa mchezo Argentuna 2, Chile 1.

Kwenye kipute cha awali kwa siku hii kilichopigwa ndani ya dimba la Levs jijini Califonia, Panama iliifunga Bolivia kwa mabao 2-1,washindi walianza kujipati bao kupitia kwa mchezaji Alberto Quintero's kunako dakika ya 10 tu ya mchezo alipounganisha kwa mtindo wa "slide motion" krosi ya Blas Perez,bao lililodumu hadi mapumziko.
Kipindi cha pili Bolivi walijipapatua na kusawazisha bao kupitia kwa Juan Carlos Arce baada ya mabeki wa Panama kuzubaa kuuondoa mpira langoni mwao.Kunako dakika ya 87 Panama walihanikiza ushindi kwa kupachika bao la pili lililofungwa na mshambulizi Blas Perez.
Leo ni
MAREKANI vs COSTA RICA
COLOMBIA vs PARAGUAY
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.