Wednesday 8 June 2016

BRAZILI YA MCHAPA HAITI GOAL 7-1


Timu ya taifa ya Brazil  leo alfajiri ya June 9 2016 ilishuka dimbani kucheza mchezo wake wa pili wa michuano ya Copa America dhid ya timu ya taifa ya Haiti, katika mchezo huo Brazil ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 7-1.
Brazil ambao walikuwa na wachezaji wao nyota kasoro Neymar Junior, walianza kupata goli la kwanza kupitia kwa Philipo Coutinho aliyefunga magoli matatu yaani hat-trick kuanzia dakika ya 14, 29 na 90, Renato Agusto aliyefunga magoli mawili dakika ya 35 na 86, Gabriel dakika ya 59 na Lucas Lima dakika ya 57, wakati goli pekee la Haiti lilifungwa na James Marcelin dakika ya 70.
Kwa matokeo hayo Brazil wanakuwa wanaongoza katika msimamo wa Kundi B kwa jumla ya point 4 wakifuatiwa na Peru wenye point moja, hiyo inatokana na wao kutoa sare mchezo wa kwanza dhidi ya Ecuador, ushindi wa 7-1 kwa Brazil unajaribu kufuta machozi kwa upande wao, kwani walishawahi kufungwa goli 7-1 na timu ya taifa ya Ujerumani tena katika ardhi yao ya Brazil wakati wa michuano ya Kombe la dunia.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.