Thursday 9 June 2016

KIM KADASHIANA AFANYA KUFURU YA KIATU CHA LAKI 7

 MWANAMITINDO na Mtangazaji wa Kipindi cha Keeping Up With The Kardashians, Kim Kardashian hivi karibuni alimfanyia sapraizi shabiki wake baada ya kumzawadia kiatu toleo la Yeezy Boost 750 chenye thamani ya shilingi laki saba za Kibongo.

Yeezy Boost 750

  Mwanadada Kim ambaye ni mama wa watoto wawili aliozaa na mumewe ambaye ni rapa, Kanye West aliandika katika ukurasa wake wa twitter.

“Vema, leo imekuwa bahati kwako… Saizi ipi inakufaa, nimekutafutia namba 10! Msaidizi wangu atawasiliana chemba na wewe kupata mawasiliano yako na Yeezy itasafirishwa kwako.”

Kiatu cha Yeezy Boost 750 bado hakijatoka, kitatoka Juni 11, mwaka huu na Kim aliweka tangazo kwenye Twitter yake kama hamasa kwa mashabiki kwa mtu atakayetoa ‘posti’ bora ya kukitangaza.
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - 👋👼👋 Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.