Thursday 23 June 2016

RATIBA YA EURO


Baada ya mechi za makundi kumalizika jana, sasa inafuata hatua ya 16 bora ya michuano ya Euro 2016. Ni baada ya mechi kali na za kusisimua zilizoshuhudia Ureno na Ireland zikipenya dakika za mwisho .

Kuna mechi kadhaa ambazo zinaturudisha kwenye historia ya mashindano haya na zinatarajia kuwa na presha kubwa kuanzia kwa wachezaji, mabenchi ya ufundi na hata mashabiki pia.

Italy v Spain inatarajiwa kuwa mechi kali mchezo ambao unazirejesha timu hizo kwenye kumbukumbu ya mchezo wa fainali ya Euro 2012 ambao Spain walishinda kwa bao 4-0.

Spain pia iliifunga Italy kwenye michuano ya Euro 2008, kwa hiyo Italy vichwani mwao watakuwa na kibarua cha kulipa kisasi watakapokutana siku ya Jumatatu.

Ufaransa v Ireland ni game nyingine ianayotazamwa kwa uzito wa aina yake licha ya Ireland kuonekana kama vibonde mbele ya Ufaransa. Goli la mkono la Thierry Henry bado linawakumbusha machungu Ireland pale waliposhindwa kufuzu kucheza michuano ya kombe la dunia.

Ratiba kamili ipo kama ifuatavyo:

Switzerland v Poland (Jumamosi)

Wales v Northern Ireland (Jumamosi)

Croatia v Portugal (Jumamosi)

France v Republic of Ireland (Jumapili)

Germany v Slovakia (Jumapili)

Hungary v Belgium (Jumapili)

Italy v Spain (Jumatatu)

England v Iceland (Jumatatu)
Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.