Tuesday, 24 January 2017

Masaa machache tu Baadaya kuapishwa Trump aanzisha bifu na Dunia nzima

Wednesday, January 25, 2017

Rais wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kutia saini sheria  kuweka masharti kuhusu wahamiaji wanaoingia nchini humo.

Taarifa kutoka Marekani zinasema ataanza kwa hatua ya kuimarisha usalama katika mpaka wa nchi hiyo na Mexico atakapozuru makao makuu ya wizara ya usalama wa ndani leo  Jumatano.

Aidha, anatarajiwa pia kutoa tangazo la kuidhinisha sheria kali zaidi za kupata visa kwa wageni kutoka eneo la Mashariki ya Kati na Afrika ambayo yana Waislamu wengi

Bw Trump ameandika kwenye Twitter kwamba leo itakuwa siku muhimu sana kwa usalama wa taifa la Marekani.

Wakati wa kampeni yake ya urais, Donald Trump aliahidi kufanyia mageuzi suala la uhamiaji Marekani.

Aligusia ujenzi wa ukuta kati ya Mexico na Marekani kuzuia wahamiaji haramu na kuwapiga marufuku Waislamu kuingia katika taifa hilo kama sehemu ya vita dhidi ya ugaidi. 

Baadaye alibadili msimamo kidogo na kufafanua kwamba watakachofanyiwa Waislamu ni kufanyiwa ukaguzi mkali kabla ya kuruhusiwa kuingia Marekani.

Anatarajiwa kufika katika wizara ya usalama wa ndani baadaye leo na anatarajiwa kusaini maagizo hayo ya kuimarisha usalama katika mpaka wa Mexico na taifa lake na baadaye wiki hiii taarifa zinaashiria atawajibikia ahadi yake ya kupunguza idadi ya wakimbizi wanaoingia Marekani.

Na hiyo ni hadi pale ukaguzi mkali utakapoanzishwa na kuzuia raia wa mataifa saba ya Afrika na kutoka eneo la Mashariki ya Kati yote yalio na idadi kubwa ya waumini wa Kiislamu.

Ubaguzi wa kidini unapigwa marufuku kwa mujibu wa katiba ya Marekani lakini inadhaniwa utawala wa Trump utaidhinisha marufuku hiyo kwa misingi kwamba ni hatua za dharura kukabiliana na tishio lililopo la ugaidi.

Awali, Bw Trump aliandika kwenye Twitter kueleza kusikitishwa kwake na kiwango cha juu cha ghasia na mauaji katika jiji la Chicago.

Vyombo vya habari wiki hii viliripoti kwamba tayari watu 228 wamepigwa risasi na wengine zaidi ya 40 kuuawa mwaka huu.

Bw Trump ameandika kwamba iwapo watawala wa Chicago hawatatua tatizo hilo la mauaji, basi atawatuma 'Feds' akimaanisha maafisa wa FBI.

Chanzo: BBC

Share:

Thursday, 29 December 2016

Simu ya Rais yatoa kelele za watu wakifanya mapenzi mahakamani

 

Moja ya habari ambazo zimeandikwa sana na vyombo vya habari vya kimataifa ni pamoja na hii inayomhusu Rais wa Bolvia Evo Morales.

Rais Evo Morales akiwa mahakamani kwenye kikao pamoja na wanasheria wa kimataifa alianza kuchezea simu yake ambapo ghafla zilisikika sauti za watu wakifanya mapenzi kwenye simu yake. Bonyeza play hapa chini kutazama

 
Share:

SHIGHATINI SEKONDARI

JE, UNA HITAJI ELIMU BORA KWA MWANAO?

 JIBU ni SHIGHATINI SEKONDARI iliyopo Usangi Mwanga Mkoa wa Kilimanjaro, inawatangazia nafasi za masoo kwa mwaka 2017/2018 kwa wanafunzi wa bweni na kutwa. wote wanaonza form one 2017 na WANAO HAMIA KIDATO CHA PILI, TATU NA NNE

ADA zetu ni nafuu kabisa, kuna mazingira mzauri ya kusomea, na hosteli zipo

mawasiliano
    0784974098 au
    0715974098


  SHIGHATINI SEKONDARI KILICHO BORA ZAIDI..

      "NYOTE MNAKARIBISHWA"

Share:

Friday, 11 November 2016

CEO
KARIBU MVUNGIPLUS  UJIPATIE DONDOO MOTO MOTO NA MAKALA ZINAZOGONGA VICHWA VYA WENGI.

TUNATOA HUDUMA ZIFUATAZO

1. ELIMU YA BIASHARA
2. USHAURI WA MAISHA
3. TUNAUZA NA KUKOPESHA MAWAZO YA BIASHARA
4. UUZAJI ZA VITABU
5. HUDUMA YA USAFIRISHAJI MIZIGO
6. MOTIVATIONAL TALKS.


           TUNAPATIKANA KWA SIMU

0762 198234/ 0719050552/ 0787000146
          BARUA PEPE
mvungifamily@gmail.com

HUDUMIWA KILA MARA


Share:


  WANAJANGWANI WATOA RAMBIRAMBI ZA KIFO CHA MBUNGE  ALI TAHIR

Uongozi wa klabu ya soka ya Yanga unasikitika kutangaza kifo cha mwanachama wake Mhe Hafidh Ally Tahir kilichotokea mjini Dodoma tarehe 10/11/2016.

Mhe Hafidh Ally Tahir – ambae Pia alikuwa mbunge wa CCM Jimbo la Segerea Dimani Zanzibar amefariki akiwa anapitiwa matibabu katika hospital ya General mkoani Dodoma.
Mheshimiwa Hafidh Ally Tahir alikuwa ni miongoni mwa Marefa wa mwanzo wa FIFA barani Afrika ambapo amechezesha mechi za soka za kimataifa.

Katika maisha yake, Mheshimiwa Hafidh Ally pia alikuwa mtangazaji wa iliyokuwa Redio Tanzania ambapo miongoni mwa manguli aliyofanya nayo kazi ni Marehemu David Wakati “Magunia”.

Katika utawala wa Rais wa Tano wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ); Mheshimiwa Hafidh Ally alikuwa Msemaji Mkuu wa Serikali, Aidha Mheshimiwa Hafidh Ally ashawahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Rahaleo.

Mheshimiwa Hafidh Ally alikuwa ni mwanasoka hadi dakika ya mwisho kwani alichezea timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Yanga iliyoinyuka ile timu shindani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Simba, ambapo alifunga magoli matatu katika mechi hiyo.

Siku moja kabla ya mauti kumfika Mheshimiwa Hafidh Ally alichaguliwa kuwa Katibu wa Timu hiyo ya Bunge, chini ya Uenyekiti wa Mbunge wa Kilolo Mheshimiwa Mwamoto.

Mchango wake Mkubwa utakumbukwa daima na sote tunaungana na familia yake, wananchi wa jimbo la Dimani chini ya Mwakilishi Mheshimiwa MwinyiHaji Makame Mwadini, Wazanzibari wote chini ya Kiongozi wetu Dkt Ali Mohamed Shein – Rais Wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na pia Watanzania wote chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli.

Yanga inatuma salamu za rambirambi maalum kwa Waheshimiwa Wabunge wote na Watumishi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Uongozi Mahiri wa Mheshimiwa Job Ndugai (Mb) – Spika wa Bunge.
Uongozi was Yanga utashiriki kikamilifu katika mazishi huko visiwani Zanzibar.

Imetolewa na Uongozi,
Young Africans Sports Club
Share:

Tuesday, 27 September 2016

Familia ya Diamond Yaikacha Sherehe ya Birthday ya Zari Iliyofanyika Zanzibar...Mabifu Yaibuka Upya

Familia ya Diamond Yaikacha Sherehe ya Birthday ya Zari Iliyofanyika Zanzibar...Mabifu Yaibuka Upya

MWISHONI mwa wiki iliyopita (juzi Ijumaa usiku) ilifanyika pati ya kusherehekea kuzaliwa kwa mpenzi wa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari’ ambayo imeibua mabifu upya. Pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa wachache kutoka Bongo ambao ni pamoja na Moze Iyobo, Aunt Ezekiel na wengineo ilifanyika Zanzibar ambapo licha ya kufana, imeibua mtifuano upya kati ya Zari na wifi yake, Esma Abdulkadiri na Diamond na mume wa zamani wa Zari, Ivan Semwanga.
 
IVAN NA DIAMOND
Bifu la wawili hawa lilikuwa limezimika, lakini lilirudi upya baada ya juzikati Diamond kumzawadia Zari nyumba iliyopo Afrika Kusini kisha kumrushia Ivan dongo kwa kuandika mtandaoni: “Wanakazana kujisifu matajiri ilhali watoto wao wanaishi kwenye nyumba za kupanga… halafu leo yuleyule wanayemtukana kutwa kwenye mitandao kuwa maskini, kajawa na shida, kanunua nyumba kulekule kwao ili watoto wao waishi maisha bora kama wanayoyatamani… Heri ya siku ya kuzaliwa Mama tee wangu…. Nakupenda sana na unalifahamu hilo…natumai umeipenda nyumba yetu hii mpya South Africa.”

NI DONGO KWA IVAN
Ujumbe huo moja kwa moja u l i o n e k a n a kumhusu Ivan ambaye kipindi cha nyuma kwa kushirikiana na mshikaji wake aliyefahamika kwa jina la King Laurence, walikuwa wakimtusi wakimsema kuwa ni maskini ila wao wana pesa licha ya madai kuwa, nyumba wanayoishi watoto wa Zari kule Sauzi ni ya kupanga. Baada ya dongo hilo, hali ilichafuka huku Ivan akimrushia madongo Diamond sambamba kumtaka Zari amwambie bwana wake (Diamond) aondoe ujumbe huo mtandaoni kwani hata wanaye wakiuona wataumia. Inadaiwa kuwa, licha ya Ivan kuomba hivyo, Zari alimjibu kuwa Diamond amegoma kwa maelezo kwamba, wao (King Laurence na Ivan) ndiyo walioanza kumtusi.

 ESMA NA ZARI
Bifu lao lilihusishwa baada ya Esma kuulizwa sababu za kutomuwish wifi yake katika siku yake ya kuzaliwa, kuonesha ‘analo na limemfika hapa’ alifunguka: “Siwezi kumuwishi, mbona Taraj (mwanaye) hakumuwishi wakati ndiye aliyekuwa akicheza na mwanaye (Tiffah) nyumbani? Wee ukosane na mimi umkasirikie hadi mtoto, ujinga huo. Siwezi kumuwishi Mbona Bi. Snura (mama wa Diamond) alimuwishi akamfuta na mafumbo juu, akasababisha watu wakamchamba!….. (anataja jina la mwandishi) nimekaa tumboni kwa mama yangu miezi 9 ‘so’ mtu anavyomletea dharau siwezi kumpenda. Mbona wote tumekaa nao vizuri haijawahi tokea haya mambo, kwa nini yeye?” alihoji Esma.

FAMILIA YA DIAMOND YASUSA BETHIDEI
Katika kile kinachoonesha kuna kitu kizito nyuma ya pazia kati ya Zari na ndugu wa Diamond, inadaiwa hakuna hata mmoja aliyefika hali iliyoibua maswali mengi.

DIAMOND, ZARI VIPI?
Kufuatia kuibuka kwa mabifu hayo sambamba na figisu nyingine, gazeti hili lilifanya jitihada za kuwatafuta Diamond na Zari kupitia simu zao za mkononi ili waseme lolote, lakini simu zao hazikuweza kupatikana.
Share:

Zitto Kabwe: Serikali ya CCM ionyeshe kuwa inawajali Wananchi wake Kuliko inavyowapenda Mafisadi wa PAP.


Monday, September 26, 2016

Zitto Kabwe: Serikali ya CCM ionyeshe kuwa inawajali Wananchi wake Kuliko inavyowapenda Mafisadi wa PAP.

NCHI HAINA DAWA MAHOSPITALINI, SERIKALI NA PAP WANAHAHA KUFUJA MABILIONI YA WATANZANIA

Gazeti la The Citizen limeandika Juu ya Suala la Ukosefu wa Madawa Katika Hospitali zote Nchini. Hii ni Habari Mbaya na Kuogopesha Kwa Watanzania Wote.

Sababu Kubwa ya Kukosekana Kwa Madawa kwenye Mahospitali nchi Nzima ni Serikali kukosa Fedha. Serikali imeipa Bohari Kuu ya Dawa nchini (MSD) 32% Tu ya Fedha ambazo ilipaswa kutoa Kwa MSD. Serikali ilipaswa kutoa Shilingi Bilioni 62.5 Kwa MSD Katika Kipindi cha Mwezi Julai mpaka Septemba 30. Lakini mpaka Leo imeipa MSD Kiasi Cha Bilioni 20 tu.

Uchunguzi Umeonyesha mpaka Septemba 16 MSD walikuwa na Tembe za Vidonge vya Paracetamol 170,000 Tu Katika Bohari Yao ya Mbeya. Huku Nchi Hospitali zikiwa hazina Kabisa Tembe Hizo. Hali ikiwa Ni Hivyo Hivyo Hivyo Katika Dawa za Ukimwi (ARVs), Vifaa Tiba kwaajili ya Mama Na Mtoto, Dawa za kipindupindu nk.

Katika Wakati ambao imegundulika tumelipa Kampuni ya Kitapeli ya PAP kwenye Sakata la Escrow zaidi ya Dola Milioni 245 Sawa Na Shilingi Bilioni 530 - Kiasi hiki Cha Fedha Ni zaidi ya Mara Mbili ya Bajeti ya Shilingi Bilioni 251 ya MSD Kwa Mwaka. Na tukilipa Bilioni 320 tunazodaiwa Baada ya Hukumu ya ICSID tutakuwa tumelipa zaidi ya Mara Tatu ya Bajeti ya MSD Kwa Mwaka.

Serikali ya CCM ionyeshe kuwa inawajali Wananchi wake Kuliko inavyowapenda Mafisadi wa PAP.

Zitto Kabwe Ruyagwa
Septemba 26, 2016

Share:

List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017


Tuesday, September 27, 2016

List Ya Vyuo Vilivyotoa Selection Ya Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Vyuo Vikuu Mbalimbali 2016/2017


Kuona Majina Ya Wanafunzi Waliochaguliwa Chuo Kikuu 2016/2017,
 
==>Chuo  Kikuu Cha Mwalimu Nyerere   <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Udsm,duce Na Muce   <<bonyeza Hapa>> 

==>Chuo  Kikuu Cha  Tumaini Makumira    <<Bonyeza Hapa>>   

==>Chuo  Kikuu Cha Udom  <<bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo  Kikuu Cha Ifm <<bonyeza Hapa>>

==>Chuo Kikuu Marian << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Cbe        << Bonyeza Hapa>>

==>Tumaini-mbeya     << Bonyeza Hapa>> & <<hapa>>

 ==>Chuo Kikuu Mum         << Bonyeza Hapa>>

==>Chuo Mum(Diploma) <<Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Stella Maris   << Bonyeza Hapa>>

 ==>Chuo- Kampala-kiu  << Bonyeza Hapa>>

Share:

Tuesday, 6 September 2016

Naibu waziri Tamisemi,Selmani Jafo anusurika kifo ajalini Mbeya

Monday, September 5, 2016

Naibu waziri Tamisemi,Selmani Jafo anusurika kifo ajalini Mbeya

Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo amepata ajali eneo la Katela Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe Mbeya.

Ajali hiyo imehusisha gari dogo aina ta Corola iliyokuwa ikotokea Mbeya kwenda Rungwe na Naibu Waziri Selemani Jafo alikuwa akitokea Tukuyu kikazi.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja amesema katika gari Waziri walikuwa watatu, Waziri Jafo mwenyewe Katibu wake na Dereva na wote walitoka salama katila ajali hiyo.

Alisema baada ya kupata ajali hiyo walipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo walifanya uchunguzi kama wameumia kwa ndan au laa! Lakin bahat nzuri Daktari aliyewafanyia uchunguz alisema hakuumia popote ni wazima.

Alisema baada ya hapo Waziri na watu waliendelea na safari yao kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kuwahi vikao vya Bunge
Gari lililoigonga gari la Naibu Waziri likiwa limetupwa korongoni.
Askari wa usalama barabaran wilayani Rungwe, Mbeya wakipima ajali ilivyotokea
Share:

Monday, September 5, 2016

Naibu waziri Tamisemi,Selmani Jafo anusurika kifo ajalini Mbeya

Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo amepata ajali eneo la Katela Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe Mbeya.

Ajali hiyo imehusisha gari dogo aina ta Corola iliyokuwa ikotokea Mbeya kwenda Rungwe na Naibu Waziri Selemani Jafo alikuwa akitokea Tukuyu kikazi.

Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja amesema katika gari Waziri walikuwa watatu, Waziri Jafo mwenyewe Katibu wake na Dereva na wote walitoka salama katila ajali hiyo.

Alisema baada ya kupata ajali hiyo walipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ambapo walifanya uchunguzi kama wameumia kwa ndan au laa! Lakin bahat nzuri Daktari aliyewafanyia uchunguz alisema hakuumia popote ni wazima.

Alisema baada ya hapo Waziri na watu waliendelea na safari yao kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kuwahi vikao vya Bunge
Gari lililoigonga gari la Naibu Waziri likiwa limetupwa korongoni.
Askari wa usalama barabaran wilayani Rungwe, Mbeya wakipima ajali ilivyotokea
Share:

Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

Powered by Blogger.