Saturday 11 June 2016

WATUMISHI HEWA 12,246 WAFUKUZWA KWENYE KAZI ZA SERIKALI


WATUMISHI 12,246 wameondolewa kwenye mfumo wa malipo ya mishahara kwa sababu mbalimbali, ikiwemo umri wa kustaafu kwa lazima, kufukuzwa kazi, vifo na kumalizika kwa mikataba.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Angela Kairuki alisema kuondolewa kwa watumishi hao kumeokoa Sh bilioni 25 ambazo zingelipwa kwa watumishi hao.

Alisema kuwa fedha hizo zingepotea endapo watumishi wasingeondolewa kwenye mfumo, ikilinganishwa na watumishi 10, 295 walioondolewa kwenye mfumo kuanzia Machi 15 hadi Aprili 30 mwaka huu.

“Jumla ya Sh bilioni 23.2 ziliokolewa kwa kipindi cha Machi 15 hadi Aprili 30 mwaka huu baada ya Rais John Magufuli kutoa maagizo ya kuwaondoa watumishi hao kwenye malipo,” alisema Kairuki. Alisema pia kuwa watumishi hewa 1,951 wameongezeka ikiwa ni pamoja na Sh bilioni 1.8.

Alifafanua kuwa ofisi hiyo ilitoa maelekezo kwa Makatibu Wakuu, Wakuu wa taasisi za umma na Mamlaka za Serikali za Mitaa, kuwasilisha taarifa ya watumishi hewa ifikapo juzi (Juni 10 mwaka huu).

Alisema kuwa walielekeza taarifa zibainishe majina, namba za hundi za watumishi hewa, tarehe walizotakiwa kuondolewa kwenye mfumo, kiasi cha fedha kilichopotea na kilichookolewa.

Akizungumzia maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Waziri huyo alisema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yatakuwa na dhana ya mchango wa watumishi wa umma katika uchumi.

Share:

0 comments:

Post a Comment


Total Pageviews

HABARI MPYA


Recent Posts Widget

CEO:KOMBO MVUNGI




HOTLINE:+255719050552 +255762198234


Email:mvungi134family@gmail.com

Dodoma,Tanzania

KARIBU UTANGAZE BIASHARA YAKO BEI NI NAFUU
Nakaribisha maoni yenu.Kama una habari pia
waweza kututumia kwenye email yetu hapo juu


Blog Archive

My Blog List

  • Happy Christmas - πŸ‘‹πŸ‘ΌπŸ‘‹ Tunawatakia happy Christmas day wadau wetu wa uhakika nakuwa ahidi juu ya kuwapatieni habari za kina katika kila nyanza, halikadhalika similizi ka...
    8 months ago
Powered by Blogger.